Showing posts with label Injili. Show all posts
Showing posts with label Injili. Show all posts
Wednesday, July 8, 2015
Tuesday, July 7, 2015
Wednesday, July 1, 2015
Maswali ya Biblia toka Injili ya Mathayo
S: Kwenye Mathayo, kuna vitu gani vinavyoitofautisha Injili hii na nyingine?
J: Mathayo anasistiza kuhusu Yesu Mfalme aliyeahidiwa, anayeanzisha ufalme wa Mungu na nu ukamilifu wa sheria. Kristo ni utimilifu wa matumaini. Kati ya waandishi wote wa Injili, Mathayo ndiye anayeonyesha vizuri zaidi jinsi ambavyo unabii wa Agano la Kale unvyotimizwa kwa Kristo. Karibu 1/3 ya Mathayo ni mahubiri, na Injili hii imepangiliwa kwa kufuata hotuba kubwa tano.
Kwa mujibu wa lugha, Papias, mwanafunzi wa mtume Yohana, alisema kuwa Injili ya Mathayo awali iliandikwa Kiebrania/ Kiaramu. Yesu ndiye "aina" ya Israeli, na wengine wanamwona Mathayo kuwa anatumia mbinu za Kimidrashi (njia ya kutafafanua Maandiko iliyotumiwa na Wayahudi wa kale yenye kuelezea mafundhisho ya kidini, kisheria na kimaadili kwa namna inayozidi maelezo halisi ya tukio husika) zilizofahamika n Wayahudi wa wakati wake.
Kuhusiana na dini za uongo, Mathayo 20:1-16 I kifungu kizuri cha kuwaeleza Wamomoni na Mashahidi wa Yehova kuhusu neema. Mathayo 18:21-35 pia inafaa kuwaonyesha Wamomoni kuwa hakuna jinsi tunavyoweza hata kuanza kumlipa Yesu kwa ajili ya neema yake kwa kutumia matendo mema.
S: Kwenye Injili ya Mathayo, inawezekanaje baadhi ya nabii zilioelezwa kwenye kitabu hiki zimuhusu Kristo?
J: Kabla ya kujibu swali, natuangalie orodha ya baadhi ya nabii zinazoongelewa kwenye swali hili.
2. Raheli anawalilia watoto wake pale Rama (Yer 31:15; Mat 2:18)
3. Unabii kuhusu Zabuloni na Naftali (Isaya 9:1, 2; Mat 4:15-16)
4. Zakaria analipwa vipande 30 vya fedha na anavitoa kwa mfinyanzi (Zek 11:12-13; Yer 32:6-9, Mat 27:9-10)
Tuesday, June 30, 2015
MAANDIKO MATAKATIFU YA KIKRISTO
Monday, June 22, 2015
INJILI YA NEEMA NA UTUKUFU WA MUNGU
Ni furaha yangu katika Kristo Yesu kutaka kuona mwili wa Kristo unapata chakula kila iitwapo Leo.
Najua kila mtu anajua nini maana ya "INJIRI" basi kwa yule am aye alikuwa hajui nini maana ya Injili ni hii.
Neno Injili linatokana na lugha ya Kiyunani.."euangelion" Maana yake.."HABARI NJEMA"
INJILI imegawanyika katika maeneo matatu.
1.INJILI YA MILELE
Hii uhusika na uumbaji wa Mungu.(Zaburi 18:1-6; Warumi 1:19-23)
2.INJILI YA UFALME.
Injili hii humdhihirisha Mungu kuwa mfalme na inasema juu ya ufalme wa Mungu hapa duniani.(Zaburi 26-12; Isaya 9:7; Mathayo 4:17; 10:5-6)
3.INJILI YA UTUKUFU
WA MUNGU
Injili hii hushuhudia wokovy katka Kristo kwa watu wote. "WAYAHUDI NA WAMATAIFA" Hapa Myahudi hana upendeleo wiwote mbele ya mtu wa mataifa. Injili hii hushirikusha "SIRI YA KRISTO" Waefeso 3:12-13 "....SIRI HIYO HAWAKUJULISHWA WANADAMU KATIKA VIZAZI VINGINE....YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI.." Injili hii inataja kwamba kanisa ni "MWILI WA KRISTO".
Injili hii itaubiliwa mpaka wakati wa "KUNYAKULIWA KWA KANISA"
Injili ya utukufu wa Mungu itatupeleka "MBINGUNI" katika katika "UTUKUFU WA MBINGUNI" kama Kristo alivyo mbinguni sasa, ndiyo maana tunashiriki baraka za ulimwengu wa kiroho.
Injili hii ya NEEMA ilianzia tangu kukataliwa kwa Israeli mpaka matengenezo yake. (Warumi 11:25-36)
Kabla ya matengenozo haya ya Israeli kanisa (tuliookoka) litanyakuliwa , na naada na hapo mabaki ya waamini wa Israeli wataanza tena kuihubiri Injili ya Ufalme, na itakuwa katika kipindi cha dhiki kuu.
Fuatana nami katika somo lijalo linalosema
WAKATI WA KUNYAKULIWA KWA KANISA LILILO MWILI WA KRISTO.
MUNGU AKUBARIKI
Subscribe to:
Posts (Atom)
