Showing posts with label Injili. Show all posts
Showing posts with label Injili. Show all posts

Wednesday, July 8, 2015

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU - SEHEMU YA PILI

I Wakorintho 14:12; ''Vivyo hivyo na ninyi kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa''.

UTENDAJI KAZI WA KARAMA.
Mambo muhimu (ya msingi) kufahamu ili karama ziweze kufanya kazi. Mambo hayo ni:-

Tuesday, July 7, 2015

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU - SEHEMU YA NNE

Karama ya unabii
I Wakorintho 12:4,10 ''Basi pana tofauti za karama bali Roho ni yeye yule. na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii, na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha.

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU - SEHEMU YA TANO

Karama ya masaidiano.
I Wakorintho 12:28; inasema '' Na Mungu ameweka wengine katika kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, na tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano na maongozi na aina za lugha''.

Wednesday, July 1, 2015

Maswali ya Biblia toka Injili ya Mathayo


Maswaliambayo huulizwa mara kwa mara kuhusu Injili ya Mathayo na Injili nyingine yanajadiliwa kwenye Mathayo au vinginevyo kwenye sehemu inayohusu Injili kwa ujumla.

S: Kwenye Mathayo, kuna vitu gani vinavyoitofautisha Injili hii na nyingine?
J: Mathayo anasistiza kuhusu Yesu Mfalme aliyeahidiwa, anayeanzisha ufalme wa Mungu na nu ukamilifu wa sheria. Kristo ni utimilifu wa matumaini. Kati ya waandishi wote wa Injili, Mathayo ndiye anayeonyesha vizuri zaidi jinsi ambavyo unabii wa Agano la Kale unvyotimizwa kwa Kristo. Karibu 1/3 ya Mathayo ni mahubiri, na Injili hii imepangiliwa kwa kufuata hotuba kubwa tano.
Kwa mujibu wa lugha, Papias, mwanafunzi wa mtume Yohana, alisema kuwa Injili ya Mathayo awali iliandikwa Kiebrania/ Kiaramu. Yesu ndiye "aina" ya Israeli, na wengine wanamwona Mathayo kuwa anatumia mbinu za Kimidrashi (njia ya kutafafanua Maandiko iliyotumiwa na Wayahudi wa kale yenye kuelezea mafundhisho ya kidini, kisheria na kimaadili kwa namna inayozidi maelezo halisi ya tukio husika) zilizofahamika n Wayahudi wa wakati wake.
Kuhusiana na dini za uongo, Mathayo 20:1-16 I kifungu kizuri cha kuwaeleza Wamomoni na Mashahidi wa Yehova kuhusu neema. Mathayo 18:21-35 pia inafaa kuwaonyesha Wamomoni kuwa hakuna jinsi tunavyoweza hata kuanza kumlipa Yesu kwa ajili ya neema yake kwa kutumia matendo mema.

S: Kwenye Injili ya Mathayo, inawezekanaje baadhi ya nabii zilioelezwa kwenye kitabu hiki zimuhusu Kristo?
J: Kabla ya kujibu swali, natuangalie orodha ya baadhi ya nabii zinazoongelewa kwenye swali hili.
1. Mungu anawaita wana wa Israel kutoka Misri (Hosea 11:1; Mathayo 2:15)
2. Raheli anawalilia watoto wake pale Rama (Yer 31:15; Mat 2:18)
3. Unabii kuhusu Zabuloni na Naftali (Isaya 9:1, 2; Mat 4:15-16)
4. Zakaria analipwa vipande 30 vya fedha na anavitoa kwa mfinyanzi (Zek 11:12-13; Yer 32:6-9, Mat 27:9-10)

Tuesday, June 30, 2015

MAANDIKO MATAKATIFU YA KIKRISTO

 








Dini iliyofunuliwa kutoka kwa Mungu ina nguvu na inakubalika sawa sawa na vile ufunuo ulivyo na nguvu na unavyokubalika. Kwa upande wa ukristo, msingi huu ambao ni mkubwa na mkuu kuliko yote ni dhaifu kabisa kutokana na kuingizwa mikono na akili za watu ndani ya Biblia. Ufunuo hauna mushkeli, tatizo ni juu ya nini kilitokea baina ya muda ufunuo ulipoteremka mpaka kipindi ufunuo huu ulipoandikwa.
Uchunguzi Makini Juu ya Agano La Kale
Wayahudi walishuhudia nyumba yao ya ibada ya Jerusalem ikiharibiwa kabisa mnamo mwaka 581 B.K. Pamoja na tukio hili pia, Torati yenyewe halisi pia iliharibiwa na baadaye walifanikiwa kurejesha hasara iliyotokea, lakini walizifanyia mabadiliko makubwa nakala chache zilizopata bahati ya kutoharibiwa kabla ya kuandika nakala nyingi zaidi kwa ajili ya matumizi ya kila mtu. Ukweli kwamba nakala chache za Agano la Kale

Monday, June 22, 2015

INJILI YA NEEMA NA UTUKUFU WA MUNGU

Bwana Yesu asifiwe!
Ni furaha yangu katika Kristo Yesu kutaka kuona mwili wa Kristo unapata chakula kila iitwapo Leo.
Najua kila mtu anajua nini maana ya "INJIRI" basi kwa yule am aye alikuwa hajui nini maana ya Injili ni hii.
Neno Injili linatokana na lugha ya Kiyunani.."euangelion" Maana yake.."HABARI NJEMA"
INJILI imegawanyika katika maeneo matatu.
1.INJILI YA MILELE
Hii uhusika na uumbaji wa Mungu.(Zaburi 18:1-6; Warumi 1:19-23)

2.INJILI YA UFALME.
Injili hii humdhihirisha Mungu kuwa mfalme na inasema juu ya ufalme wa Mungu hapa duniani.(Zaburi 26-12; Isaya 9:7; Mathayo 4:17; 10:5-6)

3.INJILI YA UTUKUFU
WA MUNGU
Injili hii hushuhudia wokovy katka Kristo kwa watu wote. "WAYAHUDI NA WAMATAIFA" Hapa Myahudi hana upendeleo wiwote mbele ya mtu wa mataifa. Injili hii hushirikusha "SIRI YA KRISTO" Waefeso 3:12-13 "....SIRI HIYO HAWAKUJULISHWA WANADAMU KATIKA VIZAZI VINGINE....YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI.." Injili hii inataja kwamba kanisa ni "MWILI WA KRISTO".

Injili hii itaubiliwa mpaka wakati wa "KUNYAKULIWA KWA KANISA"
Injili ya utukufu wa Mungu itatupeleka "MBINGUNI" katika katika "UTUKUFU WA MBINGUNI" kama Kristo alivyo mbinguni sasa, ndiyo maana tunashiriki baraka za ulimwengu wa kiroho.

Injili hii ya NEEMA ilianzia tangu kukataliwa kwa Israeli mpaka matengenezo yake. (Warumi 11:25-36)
Kabla ya matengenozo haya ya Israeli kanisa (tuliookoka) litanyakuliwa , na naada na hapo mabaki ya waamini wa Israeli wataanza tena kuihubiri Injili ya Ufalme, na itakuwa katika kipindi cha dhiki kuu.
Fuatana nami katika somo lijalo linalosema
WAKATI WA KUNYAKULIWA KWA KANISA LILILO MWILI WA KRISTO.
MUNGU AKUBARIKI